Star Tv

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba amewataka wanachama wa chama hicho kuunganisha nguvu katika kudai uchaguzi huru na haki pamoja na tume huru ya uchaguzi.

 Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya chama hicho na vyama vingine saba vya upinzani kutangaza kujitoa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa juma.

 Lipumba amewataka wanachama wa CUF kutokata tamaa kwa yote yaliyojitokeza kwenye mchakato huo.

 Mwenyekiti huyo wa CUF ameitaka kamati ya utendaji ya taifa kuendelea na kazi ya kuandaa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020 itakayojipambanua katika sera za haki na usawa .

Wakati Prof. Lipumba akitoa msimamo huo wa CUF, bado kuna mazungumzo ya ndani baina ya vyama vya siasa vya upinzani vilivyojitoa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, mazungumzo ambayo bado haijajulikana hatima yake.

                                                                                    Mwisho.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.