Star Tv

Wananchi wa kata tatu  za Matambalale ,Namikulo  na Namileme wilayani Ruangwa mkoani Lindi wamelipwa fidia ya zaidi ya Shilingi Bilioni 4 ili kupisha mradi mkubwa wa uchimbaji madini aina ya Bunyu

Mgodi huo  unaomilikiwa na  Lindi jumbo ni miongoni mwa migodi sita ya uchimbaji madini aina ya Bunyu wilayani humo .

Baadhi ya wananchi waliolipwa fidia ili  kupisha uchimbaji huo wameiomba serikali iwape kipaumbele  cha kupata ajira pindi mgodi utakapoanza kufanya kazi

Mkuu wa wilaya ya Ruangwa Hashimu Mgandilwa   amewataka wakazi wa wilaya hio kujitokeza kwa wingi  kuchangamkia fursa pindi watapo tangaza nafasi za ajira

Mgodi  huo wa uchimbaji madini aina ya Bunyu  utakapo kamilika unatarajiwa kuajiri zaidi ya  watu elfu tatu

Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.