Baada ya uchaguzi wa hapo jana, majimbo ya Brandeburg na Saxony mashariki mwa Ujerumani yanaelekea kuunda serikali za vyama vitatu.
Katika jimbo la Brandenburg, waziri mkuu Dietmer Woidke anatazamiwa kuipanua serikali ya chama chake cha SPD pamoja na kile cha mrengo wa shoto kwa kukijumlisha chama cha Kijani. Na katika jimbo la Saxony ambako chama cha CDU chini ya waziri mkuu Michael Kretschmar kimeongoza na SPD, vyama hivyo vinatazamiwa kuungana na chama cha Kijani. Mfungamano na chama cha kijani katika serikali za majimbo hayo sasa ni wa lazima ili kuzuia ushiriki wa chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD katika serikali. Katika uchaguzi wa jana chama hicho cha mrengo mkali wa kulia kilishika nafasi ya pili katika majimbo yote mawili. Hata hivyo chama cha CDU kilishika nafasi ya kwanza katika jimbo la Saxony na chama cha Social Demokratik kiliongoza katika jimbo la Brandenburg.
CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW