Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura amemweka ndani kwa muda wa saa 24 mtendaji wa kijiji cha Mau kata ya Mbulima John Ndasi baada ya kuzitafutana fedha za vitambulisho vya wajasiliamali kiasi cha shilingi milioni moja na elfu themanini.
Kumekwepo na changamoto ya baadhi ya watendaji kuto rejesha fedha za vitambulisho vya ujasilimali licha ya kutoa vitambulisho kwa wafanyabishara na kupatiwa fedha na hivyo kupelekea uongozi wa wilaya hiyo kuanzisha oparesheni ya ukaguzi wa vitambulisho hivyo kupitia kwa watendaji na kubaini baadhi ya watendaji kula fedha hizo kinyume na utaratibu.
Akiongea kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo katibu tawala wilayani humo Frank Schalwe, amesema wamelazimika kuchukua hatua ya kumweka ndani mtendaji wa kijiji cha Mau baada ya kula fedha za vitambulisho kiasi cha shilingi million moja na elfu themani.
Mkurugezi mtendaji wa halmashauri hiyo Msongela Palela amewaonya watendaji kuacha tabia ya kuzitumia fedha za vitambulisho katika matumizi yao binafus na kusema atakae bainika hatua kali za kishera dhidi yake zitachukuliwa.
Aidha Msongera amewataka watendaji kuwa wabunifu husunai wakati wa ukusanyaji wa fedha hizo kwa lengo la kuondokana na matatizo yasio kuwa ya lazima.
Hata hivyo serikali ilitoa vitambulisho elfu , 13250mia mbili hamsini na huku mpaka sasa vitambulisho 3065 vikiwa vimetolewa kwa wafanyabiashara.