Star Tv

Mkuu  wa  wilaya  ya  Kalambo Julieth Binyura  amemweka ndani  kwa muda  wa  saa 24 mtendaji  wa  kijiji cha  Mau kata ya Mbulima John Ndasi baada ya kuzitafutana fedha za vitambulisho vya wajasiliamali kiasi cha shilingi milioni moja na elfu themanini.

Kumekwepo na changamoto ya baadhi ya watendaji  kuto rejesha  fedha za vitambulisho  vya ujasilimali licha  ya kutoa  vitambulisho  kwa wafanyabishara na kupatiwa fedha  na hivyo kupelekea uongozi wa  wilaya  hiyo  kuanzisha  oparesheni  ya  ukaguzi wa vitambulisho hivyo kupitia  kwa  watendaji  na kubaini  baadhi  ya  watendaji  kula fedha hizo kinyume  na utaratibu.

Akiongea  kwa  niaba ya mkuu wa wilaya  hiyo katibu  tawala wilayani  humo Frank Schalwe, amesema wamelazimika  kuchukua hatua  ya  kumweka  ndani  mtendaji  wa kijiji cha Mau baada ya kula fedha  za  vitambulisho kiasi cha shilingi million moja na elfu themani.

Mkurugezi  mtendaji wa halmashauri hiyo Msongela Palela amewaonya watendaji kuacha tabia ya kuzitumia  fedha  za vitambulisho  katika  matumizi   yao  binafus  na  kusema  atakae  bainika  hatua kali za kishera  dhidi  yake  zitachukuliwa.

Aidha  Msongera  amewataka  watendaji  kuwa  wabunifu husunai  wakati  wa ukusanyaji  wa  fedha  hizo  kwa  lengo  la  kuondokana na matatizo  yasio kuwa  ya lazima.

Hata  hivyo  serikali  ilitoa  vitambulisho elfu , 13250mia mbili hamsini  na  huku  mpaka sasa vitambulisho 3065 vikiwa  vimetolewa  kwa  wafanyabiashara.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.