Star Tv

Raundi ya pili ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika, AFCON, itaanza Ijumaa baada ya kumalizika kwa raundi ya kwanza Jumanne na timu 16 kufuzu raundi ya pili zikiongozwa na wenyeji Misri.

Mechi za kwanza Ijumaa zitakuwa baina ya wawakilishi pekee wa Afrika Mashariki, Uganda, dhidi ya Senegal katika uwanja wa Cairo International. Pambano jingine siku hiyo litakuwa baina ya Morocco na Benin katika uwanja wa Al- Salaam mjini Cairo.

Katika raundi hiyo ya pili ambayo itakuwa katika mtindo wa mtoano wenyeji Misri watachuana na Afrika Kusini, DRC itapambana na Madagascar timu ambayo ilikuwa "Cinderella" wa fainali hizi, timu ambayo imeingia katika fainali hizo kwa mara ya kwanza na kushinda kundi lake kwa pointi saba ikiwa ni pamoja na kuifunga timu ngumu ya Nigeria 2-0 katika raundi ya kwanza.

Mechi nyingine za raundi ya pili ni Ghana dhidi ya Tunisia, Mali na Ivory Coast, Algeria dhidi ya Guinea na Nigeria itapambana na Cameroon katika moja ya mechi inayotazamiwa kuwa kali katika raundi ya pili.

Timu za Afrika Mashariki, Tanzania na Burundi zilimaliza mashindano kwa kufungwa mechi zote tatu wakati Kenya ilishinda mechi moja dhidi ya Tanzania na kufungwa na Senegal na Algeria.

Robo fainali za mashindano haya zitaanza Julai 10 na nusu fainali zitakuwa Julai 14 wakati mechi ya fainali ya mwisho itachezwa Julai 19

 

CHANZO: VOA Swahili

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.