Star Tv

Zaidi ya asilimia 80 ya  watoto  wenye umri wa chini ya miaka mitano, wamepatiwa chanjo ya  Surua Rubella  katika halmashauri ya Wilaya ya Singida kwa kipindi cha kuanzia Januari  hadi  machi mwaka huu.

Mratibu wa Chanjo katika halmashauri hiyo Emmanuel Mawa anasema kuwa kwa kipindi hicho walilenga kuchanja watoto 2,648 lakini wakafanikiwa kuwapatia huduma hiyo watoto 2,345 sawa na asilimia 89, mbali na surua rubella, pia penta wametoa chanjo ya  penta kwa  watoto 2,571 sawa na asilimia  97 kwa lengo la kuwafikia watoto 2,648 na kuwapatia huduma hiyo ya chanjo bure. Hata  hivyo amesema kuwa licha ya mafanikio hayo,  lakini  bado kuna changamoto ya  baadhi ya wazazi na walezi  kutojitokeza kuwapeleka watoto wao kwenye chanjo za aina mbalimbali, hali inayosababisha malengo yanayowekwa na halmashauri katika utoaji wa huduma hiyo kutofikiwa kwa asilimia 100.Wawa ametoa mwito  kwa wazazi na walezi kuachana na  imani  potofu na  kujenga utamaduni wa kuwapeleka watoto wao kwenye chanjo ili waweze kupata huduma hiyo kwani inatolewa bila malipo  na ni salama na muhimu kwa ajili ya kuwakinga watoto dhidi ya  magonjwa mbalimbali hatari.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.