Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya limefanikiwa kukamata Silaha moja aina ya SMG na risasi Nne na kuua Mtu Mmoja aliyefaamika kwa jina la Bahati Nyakiha anayedaiwa kuwa jambazi Sugu Mkazi wa Kijiji cha Nyarero baada ya kurushiana Risasi na Polisi katika Maeneo ya Nkerege Wilayani Tarime Mkoa ni Mara.
Hayo yamebainishwa na Kamanda Henry Mwaibambe kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya ameongeza kuwa pia Wanashikilia watuhumiwa wanane wanaodaiwa kujihusisha na suala la Wizi wa Mifuko kata ya Kitembe Wilayani Rorya na watafikishwa mahakamani ili kujibu shitaka linalowakabili.