Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo katika baraza la mawaziri.
Mabadiliko madogo katika baraza la mawaziri ni pamoja uteuzi mpya wa mawaziri watatu kwa kutengua waliokuwepo pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi.
Miongoni mwa sura mpya katika baraza hilo la mawaziri, ni mbunge aliyemteua siku chache zilizopita Dokta Stergomena Tax ambaye amemteua kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa nchini Tanzania.
Wizara zilizokutana na mabadiliko hayo, ni Wizara ya Habari kuondolewa, kutoka katika Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo na sasa itakuwa katika Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Rais Samia pia amemteua Dokta Eliezer Feleshi kuwa mwanasheria Mkuu wa Serikali, kuchukua nafasi ya Profesa Adelardus Kilangi aliyeteuliwa kuwa balozi.