Wanafunzi sita wa sekondari nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wamepigwa marufuku kuhudhuria shule yeyote katika taifa hilo baada ya video ya ngono waliyoshiriki kusambaa mtandaoni.
Wanafunzi hao walifukuzwa shule na waziri wa elimu Tony Mwaba.
Video hiyo ilipigwa picha nje ya shule yao iliyopo mjini Kinshasa, lakini ikiwaonesha wamevaa sare za shule.
Shule tano za wavulana na moja ya wasichana zilionekana kwenye video hiyo.
Waziri wa haki za binadamu bwana Albert-Fabrice Puela amesema marufuku hiyo inaminya haki za watoto.
#ChanzoBBCSwahili