Aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Tarime Vijijini John Heche wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameshindwa kutetea jimbo hilo tena.
Hii ni mara baada ya Mgombea Ubunge mwenzie kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwita Waitara kutangazwa kushinda jimbo hilo.
Waitara ameshinda ubunge Jimbo hilo la Tarime Vijijini kwa kupata kura 35,758 dhidi ya mpinzani wake John Heche aliyepata kura 18,757
Msimamizi wa uchaguzi amemtangaza Waitara kushinda kwa asilimia 95 dhidi ya mpinzani wake Heche aliyepata asilimia 10.