Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kupandisha mishahara kwa watumishi iwapo atapewa ridhaa yakuwa rais kwa muhula wa pili.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati akifanya mkutano katika uwanja wa TTC Korogwe mkoa wa Tanga wakati akinadi sera za chama hicho na kuomba ridhaa kwa wananchi kumchagua kuwa Rais na kuchagua wabunge na madiwani wa CCM.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, hiyo huku akisisitiza kuwa ili mipango mbalimbali iweze kufanikiwa ni lazima kujipanga kukusanya fedha na kutengeneza miundombinu.
“Maendeleo ni lazima yapangwe, bila kupangwa hakuna kitakachofanyika....Miaka mitano ilikuwa ya kujipanga ndio maana tulijenga vituo vya afya, zahanati, hospitali za mikoa”.-Dkt.Magufuli.
Mgombea Urais huyo amesema miaka mitano iliyopita, serikali imeweza kuajiri watumishi 74,000, pamoja na kuimarisha uchumi wa Tanzania.