Star Tv

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kupandisha mishahara kwa watumishi iwapo atapewa ridhaa yakuwa rais kwa muhula wa pili.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati akifanya mkutano katika uwanja wa TTC Korogwe mkoa wa Tanga wakati akinadi sera za chama hicho na kuomba ridhaa kwa wananchi kumchagua kuwa Rais na kuchagua wabunge na madiwani wa CCM.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, hiyo huku akisisitiza kuwa ili mipango mbalimbali iweze kufanikiwa ni lazima kujipanga kukusanya fedha na kutengeneza miundombinu.

“Maendeleo ni lazima yapangwe, bila kupangwa hakuna kitakachofanyika....Miaka mitano ilikuwa ya kujipanga ndio maana tulijenga vituo vya afya, zahanati, hospitali za mikoa”.-Dkt.Magufuli.

Mgombea Urais huyo amesema miaka mitano iliyopita, serikali imeweza kuajiri watumishi 74,000, pamoja na kuimarisha uchumi wa Tanzania.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.