Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson anatarajia kulihutubia Bunge huko Westminster siku ya Jumatatu.
Boris Johnson mbali na kulihutubia bunge anatarajiwa kutangaza hatua pamoja na masharti mapya ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya Corona.
Kupitia barua kwa Wabunge wa Uingereza iliyoandikwa na Mshauri wa Waziri Mkuu Edward Lister imeeleza kuwa;
"Kuongezeka kwa kiwango cha matukio katika maeneo mengine kunamaanisha kuwa kuna uwezekano kwamba maeneo mengine yatakuwa chini ya masharti zaidi”.
Aidha, kulingana na utafiti wa Ofisi ya Takwimu ya Kitaifa ya nchini humo (ONS) iliyotolewa Ijumaa imebainisha kuwa, wastani idadi ya kila siku ya visa vya maambukizi nchini Uingereza iliongezeka maradufu katika wiki moja mwishoni mwa mwezi uliopita.