Star Tv

Mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku anazungumza na mawakili wake kuhusu madai yaliotolewa na mmiliki wa Everton Farhad Moshiri kwamba aliamua kuondoka katika klabu hiyo baada ya kupata ''ujumbe wa uchawi''.

Moshiri aliuambia mkutano wa wamiliki wa hisa katika klabu hiyo kwamba Lukaku mwenye umri wa miaka 24 alipokea ujumbe huo baada ya kuzuru Afrika.

Lukaku alijiunga na United kwa pauni milioni 75 mwezi Julai baada ya kukataa kandarasi mpya Everton.

Mwakilishi wa mchezaji huyo aiambia BBC michezo kwamba uamuzi wa Lukaku haukushinikizwa na uchawi.

Msemaji huyo aliongezea: Hapendi kufuata imani kama hizo na sasa anatathmini hatua za kisheria anazoweza kuchukua.

BBC michezo inaelewa kwamba raia huyo wa Ubelgiji amekasirishwa na madai hayo.

Wawakilishi wake wanasema kuwa Lukaku alikataa kuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi katika historia ya klabu ya Everton ili kuweza kucheza katika klabu kubwa duniani.

Wawakilishi wake waliongezea: Romelu ni mfuasi wa kanisa katoliki na kwamba haamini uchawi. Hakuwa na imani na Everton mbali na mradi wa bwana Moshiri.

Hiyo ndio sababu hakutaka kutia kandarasi nyengine.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.