Timu ya Majimaji ya Mjini Songea inakabiliwa na uhaba wa shilingi Milioni 400 ili iweze kukidhi Mashindano ya Ligi kuu.
Hayo yamebainika baada ya mbunge mteule Damas Ndumbaro kuanza kutimiza Ahadi zake za kuwezesha kukuza Michezo katika Mkoa wa Ruvuma.
Mbunge Mteule wa Jimbo la Songea Damas Ndumbaro amesema ili kurudisha heshima ya Michezo Mkoa wa Ruvuma inatakiwa wana Ruvuma wote wasaidiane kwa njia zozote zile ili Majimaji ishinde katika Mechi zilizobaki.
Mwamuzi wa Kimataifa Joseph Mapunda amesema juhudi zinazoonyeshwa na Mbunge wa sasa wa Jimbo la Songea ni Mafanikio ki mchezo kwa Mkoa wa Ruvuma.
Picha na mtandao.