WANAWAKE nchini wametajwa kuwa ni nguzo imara katika ukuaji wa uchumi, kwa madai kuwa harakati zao ni chachu ya maendeleo, na hivyo kutakiwa kujikita katika shughuli zenye faida kubwa, ili gurudumu hilo la maendeleo kuuelekea uchumi wa viwanda lisukumwe kwa nguvu ya pamoja na watanzania wote.
Ni wanawake wajasiriamali wadogo wa mjini Iringa, wanaojishughulisha na biashara mbalimbali za kiuchumi, huku wengi wao wakielekeza nguvu zao katika biashara ndogondogo, na sababu kuu inayotajwa na wajasiriamali kubaki katika biashara hizi duni ni uhaba wa mitaji, unaowasababishia wao kukopa katika taasisi za kifedha zenye riba kubwa ambazo zinatajwa kudumaza mitaji ya wafanyabiashara wadogo Wajasiriamali wengine matamanio yao ni makubwa lakini kikwazo hapa ni namna ya upatikanaji wa mitaji.
Zainab Nuhu Mwamwindi ni mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi UWT Mkoa wa Iringa, yeye anawahimiza wajasiriamali wanawake kamwe kutobweteka kwa kufanya shughuli hizi zenye faida kiduchu na badala yake wajitoe kimasomaso kufanya biashara kubwa.
Zainab Mwamwindi ameyasema haya wakati umoja wa wanawake UWT mkoa wa Iringa ikitoa pongezi kwa rais John Magufuli, ambapo UWT amesema inaziona jitihada mbalimbali za rais ambazo zote zimekuwa na lengo la kupigania ukuaji wa uchumi wa Taifa la Tanzania.
Picha na mtandao