Star Tv

Kikosi cha usalama barabarani mkoani Morogoro kimewatahadharisha wananchi wanaotumia usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda na kukaidi kuvaa kofia ngumu kuwa watawajibishwa ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Boniphace Mbao, ametoa tahadhari hiyo, baada ya Oparesheni maalum ya kukagua na kukamata waendesha pikipiki wanaobainika kukiuka baadhi ya sharia, wawapo barabarani hususani kupakia abiria zaidi ya mmoja, pamoja na kutozingatia uvaaji wa kofia ngumu.

Amesema tangu kuanza kwa Oparesheni hiyo mwanzoni mwa mwezi huu jumla ya pikipiki 2,214 zimekamatwa huku waendesha pikipiki 76 wamefikisha mahakamani na wawili kati yao kuhukumiwa kifungo cha miezi mitatu kila mmoja.

Victor Ayo ni mkuu wa kikosi hicho wilaya ya Morogoro anasema elimu imetolewa vya kutosha kilichobaki ni usimamizi wa sheria. Kwa mujibu wa Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa, Oparesheni hiyo itakua endelevu hadi itakapo bainika kuwa waendesha pikipiki pamoja na abiria wanazingatia sheria zinazo waongoza wawapo barabarani.

Picha na mtandao

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.