Star Tv

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema viwango vya usimamizi wa mechi katika Ligi Kuu England vimeendelea kudorora mwaka baada ya mwaka.

Hii ni baada ya klabu yake kulazwa 3-1 na Manchester City mechi ya Ligi Kuu England Jumapili .

Wenger anaamini mshambuliaji wa City Raheem Sterling alijiangusha na kupewa penalti ambayo iliwasaidia wenyeji kupata bao la pili.

Kadhalika, anaamini bao la tatu halikufaa kukubaliwa kwani lilikuwa la kuotea.

"Nafikiri waamuzi hawafanyi kazi ya kutosha," amesema Wenger.

"Viwango vinashuka kila msimu kwa sasa, na kwa jumla, haikubaliki."

Mambo yakiwa 1-0, refa Michael Oliver aliwazawadi City baada ya Sterling kuanguka alipokabiliwa na Nacho Monreal wa Arsenal.

Sergio Aguero alifunga penalti hiyo.

Baada ya Alexandre Lacazette kukombolea Gunners bao moja, Gabriel Jesus alifungia City bao la tatu lakini David Silva alikuwa amejenga kibanda ardhi ya Arsenal.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.