Mbunge wa Mtama kwa Tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM ,Nape Nnauye amesema kwamba haamini kwamba katika masuala ya kuhama chama cha siasa kwa sababau kila chama kina itikadi yake na kwamba,itikadi ni sawa na imani.
Nape ambaye amewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo alisema endapo kwenye chama chake kutakuwa na mapungufu, atayashughulikia akiwa ndani na sio kuhama chama
Amesema“Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa NDANI sio NJE“