Star Tv

Serikali ya Burundi imepiga marufuku upigaji wa ngoma katika mikutano isiokuwa rasmi ikiwemo sherehe za kitamaduni na harusi katika jaribio la kuhifadhi mila hiyo ya zamani ambayo inajuliakana kimataifa.

Makundi yote yanayotaka kufanya tamasha za kitamaduni sasa yatalalizimika kujisajili na wizara ya Utamaduni na hayataruhusiwa kupiga ngoma kando na mikutano rasmi ya serikali bila ruhusa , agizo ambalo limetiwa saini na rais Pierre Nkurunziza.

Agizo hilo pia linapiga marufuku wanawake kupiga ngoma.

Hairuhusiwi kwa wanawake kupiga ngoma.

Hatahivyo wanaweza kushiriki katika kucheza densi za kitamaduni wakiandamana na ngoma hizo, kulingana na chombo cha habari cha AFP kilichonukuu agizo hilo.

Hilo ni jaribio la kusitisha na hatua mpya ya wanawake wa Burundi kupiga ngoma.

Kitamaduni wanawake hawakuruhusiwa kupiga ngoma nchini Burundi.

Ngoma inaonekana kama yenye umbo la mwanamke.

Agizo hilo pia linasema kuwa kundi lolote litakalotaka kupiga ngoma katika nchi za ugenini litalazimika kupata ruhusa kutoka kwa wizara.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.