Star Tv

Korea Kaskazini na Kusini wameanza mazungumzo kuhusu mpango wa kutuma timu kwa mashinndano ya msimu wa baridi yanayofanyika mwezi ujao nchini Korea Kusini.

Korea Kaskazini ilikubali wiki iliyopita kutuma ujumbe kwenda kwa mashindano hayo, na kupunguza msuko suko kati ya majirani hao wawili kutokana na mpango wake wa nyuklia.

Korea Kusini kisha ikapendekeza kufanyika mazungumzo makubwa Jumatatu kuhusi kushiriki kwa Korea Kaskazini.

Lakini Korea Kaskazini badala yake ikapendekeza kuhudhuria kwa kikosi chake cha sanaa katika mashindano hayo.

Korea Kusini imekuwa ikitaka Korea Kaskazini kushirikishwa kwenye mashindano hayo yaliyopewa jina olimpiki ya amani ikisema kuwa ni fursa ya kuboresha uhusiano kati ya mataifa hayo mawili.

Pande hizo mbili zinakutana eneo linalolindwa kati ya mataifa hayo la Panmunjom ambalo pia linafahamika kama truce village.

Wajumbe wawili kutoka kila upande walitarajiwa kuhudhuria mazungumzo hayo.

Wiki iliyopita wakati wa mazungumzo ya juu kati ya nchi mbili katika kipindi cha zaidi ya miaka mwilia, Korea Kaskazini ilisema kuwa itatuma wanariodha na mashabiki kwenda kwa mashindano hayo ya olimpiki ambayo yatafanyika kati ya tarehe 9 na 25 mwezi Februari mjini Pyeongchang.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.