Star Tv

Waziri wa uchukuzi nchini Israel anataka kuchimba reli ya chini kwa chini kwenye mji wa zamani wa Jerusalem karibu na Ukuta wa Magharibi na kupewa jina la Donald Trump.

Yisrael Katz alisema kuwa anataka kumpa hushima rais huyo wa Marekani kufuatia uamuzi wake wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Ukuta wa Magharibi ndilo eneo takakatifu zaidi ambapo wayahudi wanaruhusiwa kuomba.

Reli hiyo mpya ya chini kwa chini na kituo cha treni na sehemu ya mradi wa reli ya mwendo kasi kutoka Tel Aviv ambayo inatarajiwa kuzinduliwa mwaka ujao.

Ujenzi wa awali eneo lililo karibu na Ukuta wa Magharibi ambalo hujulikana kwa waislamu kama Haram al-Sharif na kwa wayahudi kama Temple Mount imezua maandamano kutoka kwa wapalestina.Israel inautaja mji wa Jerusalem kuwa mji wake mkuu huku wapalestina wakilitaja eneo la Jerusalem Mashariki lililotwaliwa na Israel wakati wa vita vya mwaka 1967 kama mji mkuu wa taifa lake la baadaye.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.