Star Tv

Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini amepigwa risasi na kujeruhiwa na wanajeshi wenzake wakati akijaribu kuvuka kwenda Korea Kusini akipitia mpaka wenye ulinzi mali.

Mwanajeshi huyo alivukia katika kijiji cha Panmunjon, ambapo makubaliano ya kumaliza vita vya Korea yalisainiwa mwaka 1953.

Karibu watu 30,000 raia wa Korea Kaskazini wamehamia Korea Kusini tangu wakati huo lakini wengi huvuka kupitia China

Si jambo la kawaida kwa mtu yeyote kuvuka mpaka unaotenganisha nchi hizo mbili.

Hiki ndicho kisa cha nne cha mwanajeshi wa Korea Kaskazini kuvuka kupitia eneo lenye ulinzi mkali.

Korea Kaskazini na Kusini wako kwenye mzozo mkubwa tangu vimalizike vita mwaka 1953 na hakuna makubaliano rasmi ya amani yaliyotiwa sahihi kati yao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.