Star Tv
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema kuwa klabu yake haingefunga bao hata kama ingecheza kwa saa kumi baada ya upande wake kupoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Newcastle. Bao la dakika ya 65 la Matt Ritchie lilisababisha The Red Devils kushindwa kwa mara ya tano msimu huu. Sasa Manchestrer United wako nyuma ya viongozi Manchester City kwa pointi 16. "Miungu yao ya kanndanda ilikuwa wazi nao," aliseam Mourinho. "Haingewezekana leo." Meneja huyo wa zamani wa Chelsea alisema kuwa Newcastle walicheza kama wanyama kushinda nyumbani kwa mara ya kwanza tangu Oktoba. "Hisia zangu ni kuwa tungecheza kwa saa 10 na hatungefuga bao," alisema. "Tulikuwa na fursa wakati tulikuwa 0-0, alisema Mourinho, Alexis Sanchez alikuwa na fursa ya kufunga na kisha fursa zingine dakika za 20 na 25 za mwisho Free-kick ambayo ilichangia bao lake Ritchie, iliptikana wakati beki wa Manchester United Chris Smalling alilaumiwa kwa kuruka. Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.