Boeng imeanzisha maonyesho yake ya ndege huko Dubai kwa kutangaa mauzo makubwa mapya katika maonyesho hayo ya siku tano.
Ilitangaza kuwa Shirika la ndege la UAE la Emirates limeagiza ndege 40 za Boeng 787 Dreamliners, katika mkataba wa thamani ya dola bilioni 15.Mwenyeki wa shirika hilo Sheikh Ahmed bin Saeed al-Maktoum, amesema kuwa Boeng imechaguliwa badala ya Airbus A350.Emirates ndilo shirika la ndege kubwa zaidi mashariki ya kati likiwa mnunuzi mkubwa zaid ya Boeng 777 na lina ndege 165 zinazohudumu likiwa tena limeagiza ndege 164.