Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo amezindua rasmi zoezi la Ufyatuaji wa Matofali kwaajili ya ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu ambapo amewasihi Wadau na Wananchi kuunga Mkono jitiada hizo.
Katika uzinduzi huo RC Makonda ameshiriki zoezi la Ufyatuaji wa Matofali kwaajili ya Ujenzi huo.
Makonda amesema lengo la Ujenzi wa Ofisi hizo ni kuboresha Mazingira ya kufanya kazi kwa walimu ili waweze kutoa Elimu bora kwa Wanafunzi na kuongeza ufaulu.