Zimeibuka fujo kubwa katika eneo la Jangwanii kufuatia zoezi la bomoabomoa linaloendelea. Inaelezwa kuna kundi kubwa la vijana wanaosadikiwa kuwa ni miongoni mwa makundi ya wahuni wakiwa na chupa, visu na mapanga wamefunga kamba eneo lao na wamesikika wakisema wasiguse polisi.
Kadhalika kundi hilo limechoma matairi na hivyo kufanya moshi mzito kutanda katika anga la eneo hilo.
Hata hivyo kamanda wa polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa ameeleza hali imedhibitiwa na Jeshi la polisi na kwamba zoezi la Bomoabomoa linaendelea. Ameeleza hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa katika tukio hilo