Star Tv

Manchester City wanatarajiwa kutoa ofa mpya kwa mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez, 29, na wanaamini kuwa Arsenal watamruhusu raia huyo wa Chile kuondoka mwezi huu.

Sanchez yuko tayari kurejesha kima cha pauni milioni 25 kuhakikisha kuwa amejiunga na Manchester City mwezi huu. (Sun)

Arsenal watamruhusu Sanchez kuondoka ikiwa watapokea hadi paui milioni 30 na wanataka shughuli hiyo kukamilika mapema ili kuwawezesha kumtafuta mchezaji ambaye atachukua mahala pake. (Mirror)

Taarifa zinasema kuwa Sanchez huenda akajiunga na Manchester City kwa muda wa wiki moja inayokuja. (Independent)

Arsenal wamemuorodhesha mshambuajia wa Monaco Thomas Lemar, 22, kuwa nambari moja katika kuchukua mahala pake Sanchez, baada ya kushindwa kumsaini mfaransa huyo msimu uliopita.Mirror

Valencia nao wako kwenye mazungumzo na Arsenal kuhusu Coquelin. (Cadena Ser - in Spanish)

Chelsea wamesitisha mikakati kwa kumwinda beki wa Juventus Mbrazil Alex Sandro, 26, kwa sababu klabu hiyo ya Italia inataka paunia milioni 60 kwa beki huyo. (Telegraph)

Mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane, 24, anasema yuko sawa katika klabu hiyo lakini ni lazima waanze kushinda vikombe kumwezesha kubaki. (Star)

Leicester wana nia ya kumuchia mshambuliaji Kelechi Iheanacho, 21, kuondoka mwezi huu licha ya kumsani mnigeria huyo tu hivi karibu kwa pauni milioni 25. (Sun)

West Ham wanakaribia kumsaini kiungo wa kati wa England na Newcastle Jonjo Shelvey, 25, kwa pauni milioni 12. (Express)

Juventus hawatamsaini kiungo wa kati wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic, 22, kwa sababu Paris St-Germain wanataka kutoa pauni milioni 150 kwa raia huyo wa Serbia ambaye pia amewavutia Manchester United. (Il BiancoNero - in Italian)

Newcastle watamruhusu mshambuliaji raia wa Serbia Aleksandar Mitrovic, 23, kuondoka Januari lakini wanataka kurejesha pauni milioni 18 walizotumia kumnunua miezi 18 iliyopita.

Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.