Star Tv

Ulinzi umeimarishwa katika jiji kuu la Kenya, Nairobi pamoja na miji mingine mikuu Rais Uhuru Kenyatta akitarajiwa kuapishwa kuongoza nchi hiyo kwa muhula mwingine hapo kesho.

Muungano wa upinzani umetangaza kwamba hautambui sherehe hiyo na haumtambui Bw Kenyatta kama rais aliyechaguliwa na wananchi.

Kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga amepanga kuandaa mkutano mkubwa wa kuwakumbuka watu waliofariki wakati wa makabiliano kati ya wafuasi wa upinzani na polisi.

Bw Odinga na muungano wake wa National Super Alliance (Nasa) wamesisitiza kwamba mkutano huo utafanyika katika uwanja wa Jacarada, Nairobi, takriban kilomita kumi hivi kutoka uwanja wa Kasarani ambapo sherehe ya kuapishwa kwa Bw Kenyatta itakuwa inaendelea.

Polisi hata hivyo wamesisitiza kwamba hakutakuwa na mkutano mwingine Nairobi ila sherehe ya kumuapisha Bw Kenyatta.

Bw Odinga alisusia uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba baada ya kufutiliwa mbali kwa uchaguzi wa kwanza uliokuwa umefanyika tarehe 8 Agosti.

Mahakama ya Juu ilifutilia mbali uchaguzi huo wa kwanza kutokana na kesi iliyokuwa imewasilishwa na Bw Odinga.

Mwezi uliopita, ripoti ya Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu ilisema watu 37 waliuawa tangu kutokea kwa uchaguzi wa tarehe 8 Agosti.

Tume hiyo iliwatuhumu polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi wakikabiliana na wafuasi wa upinzani.

Idara za usalama nchini Kenya zimekanusha tuhuma hizo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.